• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

KAMISHNA WA UHIFADHI MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO AKUTANA NA WAHEMIWA MADIWANI NA VIONGOZI WA KIMILA KUDUMISHA UHUSIANO

Posted on: September 27th, 2024

Kamishna wa Uhifadhi wa mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Dkt. Elirehema Doriye tarehe 26 Septemba, 2024 amefanya kikao cha kuimarisha uhusiano kati ya mamlaka hiyo, viongozi pamoja na wananchi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Kikao hicho kilichohusisha Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, Madiwani wa kata zote 11 za Tarafa ya Ngorongoro, viongozi wa mila (Malaigwanan) na menejimenti ya NCAA kimelenga kujadili masuala mbalimbali kwa lengo la kuimarisha uhusiano na kutatua changamoto zilizopo ili kuimarisha shughuli za uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.


“Kikao hiki ni sehemu ya NCAA kukutana na makundi mbalimbali kwa ajili ya kuboresha uhusiano na kuainisha changamoto zilizopo ili tuzitatue na tuendelea kuimarisha shughuli za uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii hasa kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi waliopo sambamba na kuendelea kuwaelimisha kuhama kwa hiari ndani ya hifadhi” alibainisha Dkt. Doriye.

Mbunge wa jimbo la Ngorongoro Mhe. Emmanuel Ole Shangay amempongeza kamishna wa Uhifadhi NCAA Dkt Elirehema Doriye kwa kuendelea kuimarisha uhusiano na wananchi wa Ngorongoro hali inayosaidia kutatua  kero za wananchi hao sambamba na kuimarisha uhifadhi shirikishi kwa manufaa ya wananchi hao na watanzania kwa ujumla.  


Mhe. Shangay ameishukuru  Serikali kupitia NCAA na Halmashauri ya Wilaya Ngorongoro kwa kuendelea kuimarisha huduma za kijamii kwa wananchi wa Ngorongoro na kutatua changamoto za muda wa wananchi kuingia ndani ya hifadhi kutoka saa 10:30 jioni hadi saa 12 kamili jioni.


Ameinisha kuwa hakuna kiongozi anayepingana na agizo la serikali kwa wananchi wa Ngorongoro ambao wako tayari kuhama kwa hiari ndani ya hifadhi hiyo kwenda Kijiji cha Msomera na maeneo mengine yaliyotengwa na Serikali na yale wanayochagua wenyewe lakini pia amesisitiza umuhimu wa serikali kuendelea kutoa huduma kwa wananchi ambao bado hawajafanya maamuzi ya kuhama.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro Bw. Sadick Mbilu amefafanua kuwa halmashauri ya Ngorongoro itaendelea kushirikiana na NCAA  kuimarisha shughuli za uhifadhi na kutoa huduma za kijamii kama afya, elimu, maji, miundombinu na kukutana na wananchi kwa ajili ya kuwasikiliza, kutatua changamoto zao sambamba na kuendelea kutoa elimu ya kuhama kwa hiari ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili kuimarisha shughuli za uhifadhi na kuboresha Maisha ya wananchi nje ya hifadhi.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ngorongoro Mhe. Marekani Bayo ameeleza kuwa halmashauri ya Ngorongoro kupitia baraza la madiwani itaendelea kushirikiana na NCAA katika kukuza uhusiano  na kufanya uhifadhi shirikishi kupitia vijiji vyote vinavyozunguka hifadhi ya Ngorongoro na pori la akiba la Pololeti ili wananchi wanufaike na mapato yatokanayo na shughuli za utalii kwa ajili na kuiwezesha Serikali kuwahudumia.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA MIRADI YA MARNDELEO ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI WILAYANI NGORONGORO

    May 16, 2025
  • NGORONGORO MSTARI WA MBELE KUHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

    May 09, 2025
  • KISIMA CHA MAJI SAFI KUCHIMBWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA NGORONGORO

    April 25, 2025
  • ZIARA YA MWENYEKITI WA HALMASHAURI TARAFA YA NGORONGORO.

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.