Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesema Shilingi 19,513,813,347 zimetolewa ili kusambaza umeme kwenye Vitongoji 127 vya Majimbo sita ya Mkoa wa Arusha ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Rais Samia Suluhu Hassan ya kufikisha umeme kwenye Vitongoji vyote Mkoani Arusha mara baada ya kuwa Serikali imefikisha umeme kwenye Vijiji vyote 368.

Mhe. Makalla amebainisha hayo leo Jumanne Februari 04, 2026 Ofisini kwake Jijini Arusha alipotambulishwa Mkandarasi Nakuroi Investment Company Ltd, atakayetekeza mradi wa usambazaji umeme katika Vitongoji hivyo 127 kutoka katika Wilaya zote za Arusha.
“Kikubwa kwaniaba ya Wakuu wa Wilaya niwahakikishie ushirikiano Tanesco pamoja na Mkandarasi anayetekeleza mradi huu na niagize Mradi mmoja unapokamilika, uzinduliwe wananchi waanze kufaidika. Niagize pia kutumika kwa Vijana wa maeneo husika ili wapate ajira wakati wa utekelezaji wa mradi huu wa Umeme.” Amesisitiza Mhe. Makalla.
Kwa upande wake Mhandisi Erin Mhina, Mratibu wa miradi ya REA amemueleza Mhe. Makalla kuwa jumla ya wateja 4086 wataunganishwa na umeme katika mradi huu, akimshukuru Rais Samia kwa uwekezaji wake mkubwa katika miradi ya umeme Mkoani Arusha, akisema kando ya mradi huu wa sasa ipo miradi mingine 6 inayotekelezwa Mkoani hapa, yote ikigharimu Shilingi Bilioni 99.18.

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.