Kamati ya fedha, uongozi na mipango Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro leo tarehe 18 Juni, 2025 imekaa kikao na kupitia taarifa ya mapato na matumizi ya mwezi Mei 2025 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025 kuipongeza halmashauri kufanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni 374.5 na kufanya jumla ya makusanyo kuwa shilingi bilioni 3.630 sawa na asilimia 101 ya makisio ya kukusanya jumla ya shilingi bilioni 3.588.
Pia, Halmashauri ilifanikiwa kupata pesa ruzuku ya matumizi ya kawaida kutoka Serikali kuu jumla ya shilingi milioni 75,094,500 na kufanya jumla ya shilingi 2,514,420 sawa na asilimia 98, ruzuku ya mishahara shilingi 16,498,942,250 na fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo kiasi cha shilingi 16,930,744,235.
Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mohammed Bayo na kuhudhuriwa na wajumbe wa kamati ya fedha Pamoja na Wakuu na Divisheni na Vitengo.
Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.