• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI WENYE JUMLA YA TSH BILIONI 33.4 KWA MWAKA WA FEDHA UJAO 2022/2023.

Posted on: February 17th, 2022

NGORONGORO:.

16.02.2022

Baraza la Madiwani halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro  limepitisha Mpango wa Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka ujao wa fedha 2022/2023, kwenye mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani ulliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro


Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, mheshimiwa Marekani Bayo, amethibitisha baraza hilo kupitisha Mpango wa bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka ujao wa fedha kiasi cha shilingi bilioni 33.4,kwa kuwataka watalamu, kuboresha vyanzo vya mapato vilivyopo na kuimarisha mkakati wa ukusanyaji mapato huku wakiendelea kubuni vyanzo endelevu vya mapato vitakavyowezesha utekelezaji wa bajeti iliyopitishwa kiuhalisia.


"Ninawapongeza watalamu wa ngazi zote, ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ngoromgoro, waheshimiwa madiwani na wadau wote wa maendeleo kwa ushirikiano wao unaowewezesha kusukuma gurudumu la maendeleo la halmashauri yetu, licha ya changamoto nyingi lakini bado utekelezaji wa malengo ya halmashauri unafanyika kwa kasi" amesema Mheshimiwa Mwenyekiti huyo.


Aidha Mwenyekiti huyo, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuendlea kuleta fedha za  kutekeleza miradi mikubwa katika halmashauri hiyo, ikiwemo miradi ya maji, barabara, umeme, elimu na afya, miradi ambayo kupitia mapato ya halmashauri peke yake isingeweza kutekelezeka

Awali akiwasilisha Rasimu ya Mpango wa Bajeti ya Mapato na Matumizi ya kwa mwaka ujao wa fedha 2022/2023 mbele ya wajumbe wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani, Afisa Mipango halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro , Bi  Emmy Hongoli amesema kuwa, halmashauri inategemea kukusanya na kutumia jumla ya shilingi bilioni 33.4 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato.


Afisa Mipango huyo ameainisha mchanganuo wa bajeti hiyo ya bilioni 33.4 itahusisha mapato ya ndani kiasi cha shilingi bilioni 2.3 Ruzuku ya mishahara (PE) shilingi bilioni 13.5 Ruzuku ya matumizi mengine (OC) shilingi milioni 700 huku  Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo ikiwa ni shilingi bilioni 16.8


Hata hivyo Afisa Mipango huyo, amesema kuwa mpango huo wa bajeti umeandaliwa kwa mujibu wa kifungu Na. 11 cha  sheria ya Sheria ya Bajeti Na. 21 ya mwaka 2015 pamoja na Kanuni zake, maelekezo na mwongozo wa kitaifa maandalizi ya Bajeti, unaoelekeza  kupokea mapendekezo na vipaumbele kisekta kuanzia ngazi ya  vitongoji, vijiji, kata, Idara na Vitengo vya halmashauri.


Ameongeza kuwa, halmashauri imefanya Mpango wa Bajeti hiyo, kwa kuzingatia ukomo wa bajeti na kwa mujibu wa  Sheria na Maelekezo na Mwongozo wa kitaifa lakini pia imezingatia Mpango shirikishi wa Jamii, Mpango mkakati wa halmashauri wa mwaka 2021/2022  mpaka 2025/2026 na vipaumbele vya halmashauri kisekta kwa kuzingatia maeneo

Aidha Afisa Mipango Ana ameendelea kufafanua kuwa, katika mpango huo wa Bajeti umejikita pia katika kutekeleza shughuli zinazolenga kutekeleza Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania ( MKUKUTA III), inayosisitizwa na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, Mpango wa Taifa wa Miaka mitano , Malengo ya maendeleo endelevu,  (SDG's) ya 2030 pamoja na kuzingatia 'Tanzania Development Vission 2025'.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • RC KIHONGOSI AKABIDHIWA OFISI RASMI.

    June 30, 2025
  • RC KIHONGOSI AWASILI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • SERIKALI YATENGA BILIONI 11 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO SHULENI.

    June 21, 2025
  • NGORONGORO YAVUKA ASILIMIA YA MAKUSANYO MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    June 18, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.