Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mhe Raymond Mwangwala leo tarehe 15 Septemba 2023 amekagua maendeleo ya chuo cha Ualimu Ngorongoro baada ya Kupokea shilingi 413,923,764.74 kwaajili ya kukamilisha majengo saba
Aidha Mwangwala amekagua majengo 4 yakiwa katika hatua mbali mbali za Ujenzi ikiwepo bweni la wavulana ambalo linapigwa Bati na mengine yakiwa katika hatua ya Plasta.
"Tunaenda kipindi cha vuli ,Mafundi naofanha kazi hii Ongezeni kasi ya Ujenzi kabla mvua hazijazidi na kusababisha kusimama kwa kazi" Alisisitiza Mangwala
Aidha Mhandisi Mbaraka Ahmad Ally kutoka Chuo cha Ufundi Arusha anayesimamia ujenzi huo amesema kuwa mkataba wa Ujenzi wa majengo hayo unatakiwa kukamilika tarehe 30 Novemba 2023 na kuahidi kukamilisha ujenzi kabla ya tarehe ya Mkataba huo kwani kazi zote za ndani zitakuwa zimekamilika
Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.