Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mhe.Raymond Mwangwala amewaagiza watumishi wa Idara ya Afya kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kazi ili kuweza kuihudumia jamii inayowazunguka ipasavyo.
Amesema hayo tarehe 14 Septemba 2023 alipokuwa akifungua kikao cha kawaida cha utendaji na tathimini kichofanyika katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Karatu ambapo amewaonya na kuwataka watumishi kuwa na matamshi yenye lugha nzuri kwa wateja (jamii) pindi wanapowapokea na kuwahudumia huku akisisitiza madaktari na manesi (senior) wazoefu, kuwaelekeza vijana hao (Juniors) namna ya kufanya kazi na kuwasiliana na jamii wanayoihudumia.
“Kila mmoja afanye kazi kwa kufuata taratibu na kanuni kwa kuzingatia miiko ya kazi,na kuwa na nidhamu kazini” alisema Mwangala
Pia amewagiza waganga wafawidhi kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji mapato katika vituo vya kutolea huduma na Kupeleka bank Kwa usalama zaidi fedha zilizopatikana Ili baadae ziweze kuisaidia kukamilisha miradi maendeleo inayoendelea.
"Mkasimamie Mifuko wa Bima ya Afya iCHF/NHIF na mapato ya Papo kwa papo ,kuhakikisha wanachama wanajiunga na kupata Huduma,na madai ya bima yatumwe kwa wakati ili vituo viweze kupata fedha za kujiendesha"alisema Mhe.Mwangwala
Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt Revocutus Ndyekobora mewataka watumishi wote wa Idara hiyo kuheshimu Uongozi uliopo madarakani, kukubali mabadiliko yaliyopo na kuwa tayari kuendana nayo ili kuhakikisha kazi zinakwenda kama kanuni zinavyoelekeza ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa kushirikiana (team work).
“ Vunjeni makundi yanaharibu kazi ,heshimuni mamlaka iliyopo madarakani na kuitii huo ndio utumishi wa UMMA”alisema Dkt Dyekobora
Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.