Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella, amekagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Soitsumbu Losirwa -Kirtalo na Mairowa - Njoroi, zinazojengwa kwa fedha za ufadhili kutoka Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW) kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kwenye Mradi wa Uhifadhi na Maendeleo wa Mfumo wa Ikologia wa Serengeti.
"Licha ya kuwa mmeongezewa muda wa utekelezaji wa mradi, hakikisheni mnakamilisha mradi huo kwa wakati, ili kuondoa kero zinazowakabili wananchi na zaidi kutimiza adhma ya Serikali ya kuhakikisha barabara zinapitika kipindi chote cha mwaka"Amesisitiza Mhe. Mongella
Akiwasilisha taarifa ya mradi, msimamizi wa mradi huo, Mhandisi Richard Mwakasitu amesema kuwa, ujenzi huo wa barabra, unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.9, ukijumuisha ujenzi wa barabara za Soitsumb - Losirwa mpaka Kirtalo yenye urefu wa Km 12.6 na barabara ya Mailowa - Njoroi yenye urefu wa Km 11, kwa kiwango cha moramu, mradi ambao unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba 2023.
Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.