• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

JUMUIA YA TAWALA ZA SERIKALI ZA MITAA MKOANI ARUSHA(ALAT)WAFANYA ZIARA YA KUKAGUA,KUJIFUNZA NA KUSHAURI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI NGORONGORO

Posted on: December 11th, 2018

Ngorongoro  Arusha ,

Kamati  hiyo ya ALAT Mkoa wa Arusha ikiongozana na na wajumbe ilinza  kutembelea  mradi wa maji wa Mji wa Loliondo ,mradi wa rea,mradi wa barabara Wasso-Sale , Kituo cha Afya Sakala  na kuhitimisha katika kata ya Samunge kwa kukagua mradi wa Chuo cha Veta na kituo cha Afya

        Wajumbe walitembelea kituo cha afya Sakala ambapo Kaimu Mganga Mkuu (W) aliwasilisha taarifa kwa wajumbe ikionesha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro ilipokea kiasi cha shilingi za kitanzania milioni mia nne (400,000,000) tarehe 16/01/2018 kutoka Serikali Kuu kwa hisani wa Ubalozi wa Canada chini ya mfuko wa pamoja wa Afya kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Kituo cha Afya Sakala.Majengo manne yamejengwa ambayo ni jengo la upasuaji, jengo la kuhifadhia maiti, wodi ya wazazi pamoja na nyumba ya mtumishi.Hadi sasa Mradi umegharimu jumla ya tshs 433,000,000 ikiwa Tshs 33,000,000.00 ni mchango wa Halmashauri. ujenzi unaendelea na unategemea kumalizika ifikapo mwezi Januari 2019.

           Wajumbe wa ALAT walipata nafasi ya kusikiliza taarifa ya Meneja wa Mamlaka ya Maji Mji wa Loliondo ikionesha Serikali kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji, inatekeleza mradi wa majisafi ndani ya Mji wa Loliondo. Wizara imekasimu utekelezaji wa mradi huu kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira jiji la Arusha (AUWSA) kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mji wa Loliondo (LOLUWSA). Mradi huu ni miongoni mwa miradi inayotekelezwa kwa kutumia fedha za ndani kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Kazi zinazotarajiwa kufanyika katika mradi huu ni kama ifuatavyo;

  • Ujenzi wa tenki la maji lenye ujazo wa lita 225,000.
  • Ukarabati wa kisima kilichochimbwa kupitia mpango wa maendeleo wa sekta ya maji (WSDP I) eneo la Wasso kwa kununua pampu mbili.
  • Kujenga nyumba ya pampu na uzio wake
  • Kujenga mabomba ya kupandisha maji toka kwenye pampu mpaka eneo la tenki (rising main) urefu wa kilometa 3.
  • Kuendeleza mtandao wa bomba za maji (extension) urefu wa mita 11,995 na kurekebisha mtandao uliopo (rehabilitation) urefu wa mita 2,400.
  • Ukarabati wa matenki yaliyopo yenye kuhitaji ukarabati ambayo ni tenki la Makao na tenki la Ng’arwa.
  • Ununuzi na kuiunganisha mashine ya kupampu maji kutoka kwenye chanzo cha maji Ng’arwa hadi kwenye tenki la ng’arwa.

Gharama za mradi huu kwa mujibu wa mkataba ni kiasi cha Tshs. 366,082,956.33/- na Mkandarasi anayejenga mradi huu ni kampuni ya Kitibu Company Limited.

            Wajumbe walipata taarifa ya Ujenzi wa Barabara ya lami ya LOLIONDO -MTO WA MBU  ikieleza kuwa Mradi unatekelezwa kwa km 49 kuanzia Wasso hadi  Sale, mradi  ulianza tarehe 18/10/2017  na unategemewa kukamilika tarehe 17/10/2019. Gharama ya mradi mzima kwa km 49 ni Tshs. 87,126,445,712.35 ikiwa ni pamoja na VAT. Mkandarasi wa Mradi huo ni CHINA WU YI CO.LTD na ametekeleza mradi kwa asilimia 24.85%.

Vile vile wajumbe walipata nafasi ya kutembelea mradi ya usambazaji umeme vijijini REA .Kaimu Meneja TANESCO (W) aliwaeleza wajumbe kuwa Usambazaji wa umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa kwanza katika wilaya ya Ngorongoro umezinduliwa rasmi tarehe 19/08/2017 katika kata ya Digodigo na mkandarasi anayetekeleza mradi huu ni NIPO GROUP LTD.Mkandarasi alianza rasmi kutekeleza mradi huu katika Wilaya ya Ngorongoro tarehe 01/06/2018 na maeneo yanayopitiwa na mradi ni 37.Umbali wa laini za umeme utakuwa km 182 kwa msongo mkubwa wa kilovoti 11 na km 72.3 kwa msongo mdogo wa kilovoti 0.4 (400V). Hadi sasa msongo mkubwa wamevuta waya umbali wa km 14 na msongo mdogo umbali wa km 0.7, mashimo yamechimbwa km 07 kuelekea Magaiduru.

           Wajumbe wa ALAT pia walipata nafasi ya kutembele Mradi wa nyumba ya waalimu 6.1   uliofadhiliwa  na Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) na  ulitegemea kugharimu kiasi cha Tshs 141,000,000 hadi kukamilika kwake. Hadi sasa Mradi umekamilika  na umegharimu jumla ya tshs 127,988,464 tu hivyo kuwa na Bakaa ya Tshs 13,011,536.Vile vile  maabara ya Kemia katika shule ya sekondari Samunge ambayo imejengwa kwa fedha za  EP4R na ulitengewa kiasi cha Tshs. 30,000,000 na kiasi kilichotumika ni 27,000,000 ambazo zilitumika kumalizia ujenzi pamoja na kuweka vifaa katika maabara hiyo.

             Katika kata ya samunge wajumbe wa ALAT walitembeelea Mradi wa nyumba ya watumishi katika Zahanati ya Samunge ambao ulianza kutekelezwa kwa nguvu za wanawake wa Samunge kwa kuchangisha fedha kiasi cha Tshs. 10,000 kwa kila mmoja na kuweza kujenga jengo mpaka hatua ya Lenta.Aidha Mhe. Mbunge William ole Nasha alisaidia kwa kupaua jengo hilo na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro ilitoa kiasi cha Tshs. 20,000,000 kwa ajili ya umaliziaji ambapo kwa sasa mradi upo katika hatua ya umaliziaji.

           Baada ya ziara hiyo Mheshimiwa Mwenyekiti aliwashukuru wajumbe waliotembelea miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongroro na kutoa pongezi nyingi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro  kwa utekelezaji na usimamizi mzuri wa miradi hiyo kwani thamani ya fedha imeonekana.Aidha alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro kwa kushiriki kikamilifu katika kujiletea maendeleo yao na kuwaasa Halmashauri nyingine kuiga mfano wa wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro. Katika kuunga mkono juhudi za  akina mama wa Samunge wajumbe wa ALAT  walichangia walichangia kiasi cha Tshs 220,000/-

Imetolewa na 

Kitengo cha Habari na Uhusiano 

Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro Bw.Peter Juma  wateta jambo na Mkamu mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Arusha Mh. ...wakati walipotembelea mradi wa Barabara ya lami inayojengwa kutoka WAASO -SALE

 Wajumbe wa ALAT mkoa wa Arusha wakipata maelezo kutoka kwa Diwani wa kata ya Samunge baada ya kutembelea ujenzi wa chuo cha VETA


Wajumbe wa ALAT wakipata maelezo ya Mradi wa usambazaji wa Mji katika Mji wa LOLIONDO 

.Pichani ni wajumbe wa ALAT mkoa wa Arusha walipotembelea Ofisi za TANESCO wilaya ya Ngorongoro kupata taarifa ya Utekelezaji wa Usambazaji wa Umeme vijijini (REA)

Wajumbe wa ALAT mkoa wa ARUSHA walipotembelea nyumba ya watumishi katika zahanati  ya Samunge na walipaata nafasi ya kuwaunga mkono wakinamama hao kwa kuwachangia kiasi cha shilingi 220,000



Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • NGORONGORO MSTARI WA MBELE KUHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

    May 09, 2025
  • KISIMA CHA MAJI SAFI KUCHIMBWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA NGORONGORO

    April 25, 2025
  • ZIARA YA MWENYEKITI WA HALMASHAURI TARAFA YA NGORONGORO.

    April 28, 2025
  • WANAFUNZI 576 WA KIDATO CHA SITA KUFANYA MTIHANI WA TAIFA NGORONGORO.

    May 06, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.