Makamu Mwenyekiti baraza Madiwani la Hlmashauri Mhe. Emanuel Tonge ameiongoza kamati ya fedha pamoja na wataalam kutoka halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za mapato ya ndani na serikali kuu ambapo jumla ya miradi ni minne ikiwemo Zahati ya Samunge, Zahanati, Oldonyosambu, Masusu sekondari pamoja na Zahanati ya Sale.
Hata hivyo kamati imepongeza hali ya miradi ilipofikia hususani katika Shule ya Masusu sekondari, Vifaa tiba katika Zahanati ya Sale, mazingira ya maabara katika Zahanati ya Samunge na kutoa maelekezo ya kukamilika kwa miradi hususani sehemu ambazo zitakiwa kukamilika kurekebishwa ikiwemo jengo la mionzi ya Zahanati ya Sale, kukamilishwa kwa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) Zahanati ya Samunge.
Aidha kamati hiyo imetoa pongezi kwa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za miradi ya maendeleo pamoja vifaa tiba vya kisasa katika vituo vya Afya na Zahanati.
Kamati pia imetumia nafasi hiyo kutoa rai kwa watumishi wapya kuwa na uvulivu, kujituma, kuwa wabunifu na kutoa ushirikiano kwa wananchi ili kuongeza ubora wa huduma kwa jamii.
"Niwaombe watumishi WA Zahanati ya Samunge kuwa na uvumilivu katika mazingira yenu ya kazi ili muweze kuonyesha uwezo wenu. pia nawaomba mvitunze vizuri vifaa tiba mlivyoletewa ili viwasadie kutoa huduma bora kwa wananchi" amesema Mhe.Tonge
Hata hivyo kamati imeahidi kutoa kiasi cha shilingi milioni 10 katika Zahanati ya Sale ili kusaidia kuleta kiti maalumu kwa ajili mama aliyejifungua.
Kwa upande wa wananchi nao wametoa pongezi na shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita kwa kuwaletea miradi ya shule na zahanati hali inayowafanya wapate huduma za muhimu za kijamii, pia ameipongeza kamati ya fedha kwa ufuatiliaji mzuri wa miradi inayoendelea.
Ifahamike kuwa Serikali ilitoa kiasi cha Sh. 50, 000, 000 za kitanzania katika kuteleza mradi wa maabara na jengo la OPD katika zahanati ya Sale mnamo tarehe 13 Februari 2023,Kiasi cha Sh. 50, 000,000 ujenzi wa jengo la OPD zahanati ya Oldonyosambu. Na kiasi cha Sh.100,000,000 Zahanati ya Sale kwa ajili vifaa tiba vya kisasa na vifaa vyote vimenunuliwa.
Mwisho kamati ya fedha ikatoa maelekezo kwa Afisa Elimu hatua za usajili shule ya Masusu sekondari uanze mapema ili kufikia januari 2024 ianze kutumika rasmi kwani mradi huo mpaka sasa umefikia hatua ya mwisho kabisa ili kumalizika.
Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.