• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

LOLIONDO HALF MARATHON 2017

Posted on: December 18th, 2017

Mnamo tarehe 16-12-2017 kamati ya Michezo Wilaya iliandaa mashindano ya loliondo - serengeti half marathon. Lengo la mashindano haya lilikuwa kusherehekea miaka 56 ya uhuru wa Tanzania bara, kuimarisha afya, kuinua ari ya michezo Ngorongoro, kuibua vipaji mbalimbali pamoja na kuhamasisha wananchi kuhifadhi mazingira na kulinda maliasili zilizopo kwa lengo la kuendeleza utalii Ngorongoro ili tuweze  kunufaika kama wilaya pia kama Taifa. Mashindano haya yaliongozwa na kauli mbiu isemayo  tushiriki kulinda na kuhifadhi maliasili kwa pamoja ili kukuza utalii kwa maendeleo yetu. Mashindano haya yalihusisha michezo mbalimbali ikiwemo riadha  na mpira wa miguu. Kwa upande wa riadha wananchi walikimbia mbio  za kilometa 21 kwa wanaume , kilometa 10  kwa wanawake na kilometa 2.5  kwa watoto.

 Mgeni rasmi katika mashindano haya alikuwa Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro ndugu Rashid M. Taka. Mgeni rasmi aliambatana na kamati ya ulinzi na usalama na viongozi wengine akiwemo Mkurugenzi  Mtendaji  Wilaya ya Ngorongoro ndugu Raphael J. Siumbu , wakuu wa idara, watumishi wengine wa halmashauri, taasisi za umma na binafsi. Mashindano haya pia yalihudhuriwa na mwenyekiti wa CCM Wilaya.

Uzinduzi wa mbio hizo ulianza mapema asubuhi  kwa mbio za viongozi ambapo mheshimiwa Mkuu wa Wilaya  na Mkurugenzi mtendaji wa halmshauri ya wilaya ngorongoro waliongoza mbio hizo. Baada  ya hapo mashindano yalianza rasmi ambapo mbio za kilometa 21 wanaume walikimbia Kuanzia shule ya msingi wasso kupitia barabara ya  sakala hadi loliondo NMB junction na kurudi shule ya msingi wasso kupitia barabara kuu. Wanawake kwa mbio za kilometa 10 walikimbia kuanzia shule ya msingi wasso hadi shule ya msingi Mama Sara na kurudi shule ya msingi wasso nao watoto walikimbia kilometa 2.5 kwa kuzunguka uwanja wa shule ya msingi wasso. Mbali na mchezo wa riadha mashindano hayo yalishirikisha mpira wa miguu kati ya loliondo sports club na magereza sports  ambapo timu ya loliondo sports illishinda.

Washindi wa mashindano ya riadha  walikuwa kama ifuatavyo; kilometa 21 wanaume  mshindi wa kwanza alikuwa ni Rayket Gamaya (dakika 66), mshindi wa pili Wilson Ngabasi (dakika 69) na Mshindi wa tatu Yotam Gwandu (dakika 72). Kwa mbio za kilometa 10 wanawake mshindi wa kwanza Pendo Ibrahimu  (dakika 61), mshindi wa pili Tiweli Saudi (dakika 63) na  Mshindi wa tatu Penina Michael  (dakika 67).  Kilometa 2.5 kwa watoto mshindi wa kwanza ni Emanual Paul mshindi wa pili ni Monika Taiwap na mshindi wa tatu Brayson Elly. Zawadi mbalimbali zilitolewa kwa washindi zikiwemo fedha, vyeti na mipira.

Akitoa shukrani  wakati wa kufunga mashindano haya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya aliwapongeza washindi wote na kuwashukuru watu mbali mbali  kwa jinsi walivyojitoa kufanikisha mashindano haya . Pia aliishukuru halmashauri ya wilaya ya ngorongoro, GIZ na  mamlaka ya hifadhi ya  Ngorongoro kwa jinsi walivyochangia kufanikisha mashindano haya  na aliwaomba wasisite kutusaidia pale tutakapowahitaji kwani huu ni mwanzo tu wa michezo ambayo tutaendelea kuifanya na kuiimarisha ndani ya halmashauri yetu . Aidha mgeni rasmi aliahidi kuyaenzi mashindano haya na kusema kuwa mwakani mashindano haya yatasajiliwa kitaifa hivyo kushirikisha wachezaji kutoka mikoa mbalimbali na kuyafanya makubwa kuliko yanavyoonekana sasa hivyo akawataka wachezaji  wajiandae ili waweze kushindana na wachezaji wengine watakao shiriki.

Naye mwenyekiti wa CCM wilaya aliwashukuru na kuwapongeza waandaaji, wawezeshaji na wachezaji wote kwa ujumla pia  aliwaomba waandaaji kama ikiwezekana mashindano haya yawe yanafanyika kwa kata ili kupata wachezaji wengi  na bora zaidi.

Hata hivyo Mgeni rasmi alifunga mashindano haya kwa kutoa zawadi zikiwemo fedha taslim na vyeti  pamoja na mipira.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • NGORONGORO YANG'ARA MASHINDANO YA RIADHA UMITASHUMTA MKOA 2025.

    June 03, 2025
  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI CHANJO NA DAWA KINGA ZA MAGOJWA YA MINYOO NA TRAKOMA HALMASHAURI YA WILAYA YA NGORONGORO.

    May 30, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI WILAYANI NGORONGORO

    May 16, 2025
  • NGORONGORO MSTARI WA MBELE KUHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

    May 09, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.