• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAFANA WILAYA YA NGORONGORO

Posted on: March 9th, 2018

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani hufanyika tarehe 8 mwezi Machi kila mwaka. Kwa mwaka 2018 maadhimisho haya kitaifa yamefanyika mkoani Arusha na kwa Wilaya ya Ngorongoro yamefanyika kata ya Oloipiri kijiji cha Orkuyeine.

Mgeni rasmi katika maadhimisho haya alikuwa Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mh. Rashid M. Taka ambapo aliwakilishwa na Afisa Utawala na Utumishi (W) Bw. Emmanuel J. Mhando. Mgeni rasmi aliambatana na baadhi ya viongozi wengine akiwemo Afisa Maendeleo ya Jamii (W) Bi Teresia A.Irafay na Wah. Madiwani ambao ni viongozi wa Umoja wa Wanawake wa CCM- UWT (W)

Maadhimisho haya yalianza kwa mdahalo uliofanyika tarehe 7/03/2018 ambapo wanawake na wanaume walioshiriki walijadili changamoto zinazowakumba katika jamii zao, kama vile usawa wa kijinsia katika kumiliki mifugo, elimu na haki ya kuchagua/kuchaguliwa kuwa kiongozi wa ngazi mbalimbali.

Katika kilele cha Maadhimisho hayo, wanawake wametumia siku hiyo kufanya maonyesho ya bidhaa walizotengeza baada ya kupata mafunzo ya ujasiriamali kutoka Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro na mashirika yasiyo ya kiserikali kama PWC (Pastoral Womens Council), Shirika la Focus on Tanzania Society (FoTS Foundation) – chini ya ufadhili wa kampuni ya Utalii ya Tomson Safaris. Bidhaa zilizoonyeshwa ni asali, shanga, kuku, viatu vya wazi, mikanda na nguo za asili zinazotegenezwa na vikundi mbalimbali vilivyopo kweye kata ya Oloipiri na kata ya Ololosokwan.

Pia burudani mbalimbali zilisherehesha siku hiyo kupitia vikundi mbalimbali vya ujasiriamali.

Baada ya maonyesho hayo risala ilisomwa mbele ya mgeni rasmi ikionyesha shughuli walizozifanya, mafanikio na changamoto.

Mafanikio waliyopata ni pamoja na; kuunda na kupata usajili wa vikundi vya ujasiriamali, VICOBA (Village Community Bank), COCOBA (Community Conservation Bank). Kuundwa kwa jukwaa la wanawake wilaya ya Ngorongororo. Changamoto wanazopata ni uhaba wa soko, ubovu wa miundombinu na ukosefu mtaji.

Sherehe hizo zilihitimishwa na hotuba ambapo Mgeni rasmi alielezea namna wilaya ilivyojipanga kuendelea kutatua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo kama vile kuharakisha utoaji wa mikopo, kuongeza kiwango cha utoaji wa elimu ya ujasiriamali ili kuweza kuongeza ufanisi katika uzalishaji wa bidhaa zenye kumudu ushindani wa soko la kimataifa na mpango wa serikali kuelekea uchumi wa viwanda. Mgeni rasmi pia alitoa wito kwa wanaume na wadau wa maendeleo kuendelea kuwasaidia wanawake katika shughuli zao na kuachana na mila zilizopitwa na wakati zinazomkandamiza mwanamke.

Aidha Afisa Maendeleo ya Jamii (W) alitoa shukrani zake za pekee kwa mgeni rasmi kwa kumwakilisha Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, aliwashukuru watu wote wa kata ya Oloipiri kwa kufanya maandalizi na mapokezi makubwa, hasa viongozi wa kata- Mh Diwani Wilium Alais, na wenyeviti wa vijiji vya Orkuyaine, Sukenya na Oloipiri pamoja na watendaji wote wa kata na vijiji. Pia aliwashukuru Maafisa Maendeleo ya Jamii kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa pamoja na ushirikiano wanaounesha katika kazi. Pia aliwashukuru wageni wote kwa kuhudhuria kwa wingi maadhimisho hayo na kuahidi kuwa mwisho wa maadhimisho ndio mwanzo wa maandalizi ya maadhimisho mengine na shughuli zingine za uwezeshaji jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • NGORONGORO YANG'ARA MASHINDANO YA RIADHA UMITASHUMTA MKOA 2025.

    June 03, 2025
  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI CHANJO NA DAWA KINGA ZA MAGOJWA YA MINYOO NA TRAKOMA HALMASHAURI YA WILAYA YA NGORONGORO.

    May 30, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI WILAYANI NGORONGORO

    May 16, 2025
  • NGORONGORO MSTARI WA MBELE KUHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

    May 09, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.