• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

Madiwani watano waliojiuzulu kutoka CHADEMA na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ngorongoro waapishwa rasmi

Posted on: September 5th, 2018

Madiwani watano waliojiuzulu kutoka CHADEMA na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM) hatimaye wameapishwa rasmi tarehe 04/09/2018 katika ukumbi wa halmashauri.Hayo yalijiri wakati wa baraza la kawaida  la madiwani katika ukumbi wa Halmashuri ya  Wilaya ya Ngorongoro. Madiwani hao ni,Joseph Kerei seuri(Pinyinyi), Daniel A. Orkeri (Ngorongoro),sokoine Moir(Alaitole),Boniface M. kanjwel (soitsambu) na Lazaro s. saitoti(ngoile).

Aidha katika baraza hilo Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ndugu Rashid Mfaume Taka alipata nafasi ya kuhutubia baraza la madiwani  ambapo katika hotuba yake alisisitiza zaidi juu ya ukusanyaji wa mapato katika halmashauri kwani tumeanza mwaka wa fedha hivyo tunatakiwa kuanza kwa kasi kubwa.  Akitolea mfano chanzo cha uuzaji wa viwanja mheshimiwa mkuu wa wilaya alishauri kuwa viwanja vitangazwe na ramani zibandikwe katika mbao za matangazo ili wateja wachague viwanja ndipo waje walipie ada ya maombi pamoja na gharama yote ya kiwanja au walipie kidogo kidogo isipokuwa wasivuke mwaka wa fedha husika. Hii italeta uwazi na itaondoa utaratibu unaotumika sasa ambapo mteja hulipia ada ya maombi na akipata kiwanja anaweza kukaa nacho bila kukilipia kwa muda mrefu. Aliwataka watu wa idara ya ardhi waendelee kupima viwanja na waviuze vyote mwaka huu na kwa vile ambavyo havijalipiwa japo vilishagawanywa vitangazwe upya na viuzwe.

Mheshimiwa mkuu wa wilaya alisisitiza kuwa halmashauri iongeze jitihada katika lango la ngarasero na nyumba za kulala wageni ndani ya hifadhi ya ngorongoro ili kukusanya mapato ya kutosha kwani vyanzo hivi vina viashiria vingi vya upotevu wa mapato. Aidha aliwataka wataalam watumie mfumo wa kusajili wageni wanaolala katika hoteli za kitalii (lodge) unaotumiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na hifadhi ya Taifa ya Serengeti ili kupata idadi kamili ya wageni na kuongeza mapato.

Kwa upande wa elimu mkuu wa wilaya alisisitiza juu ya umaliziaji wa miradi viporo hasa ya ujenzi wa madarasa ili halmashauri iweze kujiandaa kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha tano kwa mwaka 2019.

Mheshimiwa mkuu wa wilaya alieleza kuwa mwenge wa uhuru kwa mwaka huu utapita katika maeneo ya Tarafa ya Ngorongoro hivyo waheshimiwa madiwani washiriki katika mbio za mwenge  na kuhamisisha wananchi washiriki kwa wingi.

Katika hatua nyingine baraza lilijigeuza kama kamati na kujadili ripoti ya uchunguzi juu ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali katika miradi ya ujenzi  ya kituo cha afya sakala na shule za sekondari za Digodigo, Sale, Nainokanoka na Loliondo na kasha kupendekeza kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa watumishi waliohusika katika michakato hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • RC KIHONGOSI AKABIDHIWA OFISI RASMI.

    June 30, 2025
  • RC KIHONGOSI AWASILI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • SERIKALI YATENGA BILIONI 11 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO SHULENI.

    June 21, 2025
  • NGORONGORO YAVUKA ASILIMIA YA MAKUSANYO MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    June 18, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.