• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

NAWASHUKURU WADAU WALIOIUNGA MKONO SERIKALI KUOKOA WAHANGA KARIAKOO .

Posted on: November 18th, 2024

Mhe. Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameungana na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwashukuru wadau wote pamoja na wananchi waliojitokeza kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwaokoa wahanga wa jengo la ghorofa nne lililoanguka katika Mtaa wa Mchikichi na Manyema uliopo Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Mhe. Majaliwa ametoa shukrani hizo leo alipolitembelea jengo hilo lililoanguka Novemba 16, 2024 kwa lengo la kujiridhisha na zoezi la ukoaji linaloendelea, ambalo linaongozwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi waliojitolea.


“Nawashukuru wadau wote wa sekta binafsi na sekta za umma pamoja na wananchi walioiunga Serikali mkono katika zoezi la kuwaokoa wahanga wa ajali hii kwa kujitolea vifaa mbalimbali, mitambo, magari na wataalam ambao wanashiriki katika zoezi la uokoaji linaloendelea,” Mhe. Majaliwa amesisitiza.


Mhe. Majaliwa amesema, wakati Serikali ikiendelea kujiimarisha katika idara ya maafa na uokozi kuna umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika jambo la dhalura kama hili la ghorofa kuanguka kwa ghorofa, kwani jambo hili si la Serikali pekee bali ni la watanzania wote.


“Tunakiri kwamba mchango wa wadau na wananchi ni mkubwa na umesaidia kuokoa wenzetu 84 ambao ni wahanga wa tukio hili na ninawahakikishia watanzania kuwa, zoezi la uokoaji linaendelea mpaka tutakapojiridhisha kwamba wote waliopo ndani ya jengo hili wameokolewa wakiwa hai au tumewapoteza kwa mapenzi ya Mungu,” Mhe. Majaliwa ameeleza.


 Sanjali na hilo, Mhe. Majaliwa amewashukuru wafanyabiashara wa Kariakoo kwa utulivu wao wakati huu ambao zoezi la uokoaji likiendelea na amewataka kuendelea kuwa watulivu ili kutoa fursa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea kutimiza jukumu la uokoaji wa wahanga ambao bado wapo katika jengo hilo lililoanguka. Ili kuongeza ufanisi katika zoezi la uokoaji, Mhe. Majaliwa amemuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila kufunga barabara ambazo matumizi yake yanaathiri zoezi la ukoaji, lengo likiwa ni kuruhusu mitambo kuingizwa kwa urahisi pamoja na kuwawezesha waokoaji kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi na weledi.


Aidha, amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini kumtafuta mmiliki wa jengo lililoanguka ili aanze kulisaidia jeshi la polisi katika kubaini chanzo cha jengo hilo kuanguka, na kuleta madhara yalipopelekea watu kupokeza uhai, hasara kwa wafanyabiashara na Serikali kuingia gharama.


Mara baada ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kujiridhisha na zoezi la uokoaji katika jengo hilo lililoanguka Karikakoo jijini Dar es Salaa, alielekea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja na kuwaongoza watanzania kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali hiyo

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • BARAZA LA HALMASHAURI NGORONGORO LATAMBUA NA KUZIPONGEZA SHULE ZILIZOFANYA VIZURI NA MICHANGO YA WADAU WA ELIMU, KFW, THOMSON Safaris na PWC ZAPONGEZWA. MIL 3.5 ZATOLEWA KAMA ZAWADI.

    February 21, 2026
  • TANAPA, FZS NA KFW WAUNGANISHA NGUVU KUBORESHA MIUNDOMBINU YA KISASA YA SHULE YA MSINGI SOITSAMBU.

    February 18, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI HALMASAHURI YA WILAYA YA NGORONGORO LIMEPITISHA RASIMU YA MPANGO WA BAJETI 2026/2027.

    February 13, 2026
  • UFUATILIAJI WA KINA KUFANYIKA KUBORESHA AFYA KWA WATOTO WENYE CHANGAMOTO YA LISHE.

    February 10, 2026
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2026
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2025/2026
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2023
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • Taarifa kwa Umma
  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2025/-2026
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.