• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

SERIKALI YATOA VIFAA VYA TIBA KITUO CHA AFYA SALE; MILION 370 ZATUMIKA.

Posted on: March 15th, 2024

Kituo cha Afya Sale kilichopo kata ya Sale kimepokea Vifaa vipya vya tiba kwaajili ya upasuaji kutoka Serikali kuu,  ili kufanikisha huduma ya upasuaji itakayoanza kutolewa katika kituo hicho hivi karibuni ambapo Kituo hicho kinatarajiwa   kuhudumia Wananchi kutoka Kata Malambo, Pinyinyi,  Oldonyosambu na Sale yenyewe.


Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mhe. Kanali Wilson Sakulo ameambatana na Wataalamu kutoka Halmshauri mpaka Kituo hicho cha Afya kwa ajili ya kukabidhi vifaa hivyo kisha kufanya Mkutano wa hadhara na Wananchi wa Sale ili kusikiliza na kutatua kero zao.


Aidha Mhe. Sakulo amewaeleza Wananchi mazuri yanayo fanywa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan hasa katika kuleta miradi ya maendeleo kwa kuboresha miundo mbinu ya kijamii katika kata ya Sale kuanzia sekta ya Elimu, Maji pamoja na Afya hususani vifaa vya tiba ya upasuaji ambavyo vitakwenda kutumika kusaidia maisha ya watu


"Mhe. Rais katoa milioni 370 za kitanzania kununua vifaa hivi na kuelekeza kuletwa katika Kituo hiki cha Afya, tumpongeze Rais wetu anafanya kazi kubwa kuhakikisha tunakua kimaendeleo" amesema Kanali. Wilson Sakulo

Hata hivyo wakati wa Mkutano huo Mhe. Mkuu wa Wilaya ameongezea kwa kutoa rai kwa Uongozi wa Kata na Kijjiji kuboresha na kudumisha ulinzi wa eneo zima la kituo cha Afya


"Kuanzia leo nataka ulinzi uimarishwe hapa, maana tunatakiwa kuvilinda vifaa hivi kwani vinathamani kubwa na vina tija kwetu sote" ameongeza Kanali. Sakulo


Akizungumza wakati wa Mkutano huo Diwani wa Kata ya Sale Mhe. Hamza Masedo amesema  Serikali ya awamu ya sita inajitoa sana katika kuboresha miradi ya maendeleo na katika kujali afya za Watanzania.


"Mama ameamua Sale vipelekwe vifaa vya kusaidia Wananchi wangu, mfano wazazi kujifungua, upasuaji, dawa za kutosha zinapatikana. Vifaa tulivyoletewa vinapatikana hata katika Hospitali kubwa ikiwemo Hospitali yetu ya Wilaya ya Ngorongoro"-Mhe. Masedo


Pia Mhe. Masedo amemueleza Mkuu wa Wilaya kuwa kwa kipindi cha miaka mitatu Serikali ya Mama Samia imetekeleza miradi ya maendeleo katika nyanja zote zenye thamani ya shilingi bilion 2.7.


Kwa upande wake Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ngorongoro (OCD) Alphonce Bandia ametoa rai kwa Wananchi wa Sale wanakua mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanakwenda na wale watoro wanafika shuleni kabla hatua kali za kisheria hazijaanza kuchukuliwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • RC KIHONGOSI AKABIDHIWA OFISI RASMI.

    June 30, 2025
  • RC KIHONGOSI AWASILI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • SERIKALI YATENGA BILIONI 11 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO SHULENI.

    June 21, 2025
  • NGORONGORO YAVUKA ASILIMIA YA MAKUSANYO MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    June 18, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.