• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

WAZIRI MCHENGERWA AKABIDHI MAGARI 10 TSC, 9 YAPELEKWA OFISI ZA WILAYA.

Posted on: August 13th, 2024

Ofisi ya Rais - Tamisemi


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa amekabidhi magari 10 kwa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) huku magari tisa (9) yakipelekwa katika ofisi za TSC ngazi ya Wilaya.


Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi magari hayo iliyofanyika tarehe 11 Agosti, 2024 katika Ofisi za TAMISEMI Mtumba jijini Dodoma, Waziri Mchengerwa alisema kuwa Serikali inatambua kuwepo kwa  uhitaji mkubwa wa magari katika Ofisi za TSC 139 zilizopo katika kila wilaya nchini.


Alisema kuwa magari 10 yaliyotolewa ni mwanzo  wa kuanza kuboresha mazingira ya utendaji kwa Makatibu Wasaidizi ili waweze kutekeleza mjukumu yao kwa ufanisi.


“Ikumbukwe kuwa Serikali imekwisha toa magari kwa Makatibu Tawala Wasaidizi Seksheni ya Elimu wote nchini, Wakuu wa Divisheni za Elimu Msingi na Sekondari wote na sasa tumeanza kwa Makatibu Wasaidizi wa TSC wa Wilaya,” alisema.



Alisema lengo  la kutoa magari hayo ni kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za elimu zinazofanyika katika ngazi ya shule pamoja na kuwafikia walimu katika vituo vyao ili kuwasilikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili.


Mhe. Mchengerwa alisema kuwa jukumu la usimamizi wa Elimu linahitaji uwajibikaji na usimamizi thabiti katika ngazi ya Taifa, Mikoa, Halmashauri, Kata na Shule.


Alisema kuwa pamoja na bidii, weledi, ubunifu, uaminifu na utiifu, mafanikio katika usimamizi wa elimu yanategemea pia uwezeshwaji wa vifaa na vitendea kazi ikiwemo vyombo vya usafiri.


Mhe. Mchengerwa aliongeza kuwa matarajio ya Serikali ni kuwa, magari waliyokabidhiwa yatakuwa nyenzo muhimu kwa viongozi wakiwemo Makatibu Wasaidizi  wa Wilaya katika usimamizi na ufuatiliaji wa Elimu nchini ikiwa ni pamoja na utatuzi wa kero zinazojitokeza.


Aidha , Waziri alielekeza kuwa magari hayo yatunzwe vizuri ili kuweza kuongeza ufanisi na ubora wa elimu katika utekelezaji wa majukumu ya kuwahudumia walimu ili wapite salama katika mzunguko wao wa ajira.

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • RC KIHONGOSI AKABIDHIWA OFISI RASMI.

    June 30, 2025
  • RC KIHONGOSI AWASILI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • SERIKALI YATENGA BILIONI 11 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO SHULENI.

    June 21, 2025
  • NGORONGORO YAVUKA ASILIMIA YA MAKUSANYO MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    June 18, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.