• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

WILAYA YA NGORONGORO YAONGOZA ARUSHA, ZOEZI LA UTOAJI CHANJO YA SURUA NA RUBELLA.

Posted on: February 21st, 2024

"Tulikua na Vituo vya Afya 38 ambavyo vyote vilitumika kutoa huduma ya chanjo, tumetekeleza zoezi kwa asilimia 136, tulipata jumla ya dozi 54, 020 tunaishukuru Wizara ya Afya kwa kutoa chanjo pamoja na fedha kwajili ya utekelezaji wa zoezi la utoaji chanjo"-Mratibu wa chanjo Wilaya ya

Ngorongoro


Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kuipitia Wataalamu wake ilianza rasmi zoezi la utoaji chanjo ya Surua na Rubella kuanzia tarehe 15-19 Februari, 2024 kwa Watoto wote waliyochini ya miaka mitano, mpaka kufikia tarehe Februari 19 siku ya mwisho ya zoezi jumla ya  watoto 50, 709 walifikiwa na kupatiwa chanjo ambapo ni sawa asilimia 136 zaidi ya lengo lilikusudiwa ikiwa kusudi ilikua ni kuchanja Watoto 37, 364 sawa na asilimia 100


Hata hivyo Mratibu wa chanjo Wilaya ya Ngorongoro Bw. Thomas Nchimbi amesema sababu iliyochangia kuvuka lengo tulilojiwekea ni kutokana na uhamasishaji uliyofanywa kwa Wananchi pamoja na ushiriakiano uliyotolewa na vyombo habari kama Loliondo fm, viongozi wote wa Serikali na Viongozi wa kidini wa Wilaya ya Ngorongoro


"tuna Vituo vya Afya 38 ambavyo vyote vilitumika kutoa chanjo wakati wote kwa siku nzima, tulikua na vituo vya muda 154 (kliniki ya mkoba) ambapo Wahudumu wa Afya walikwenda maeneo tofauti kutoa huduma ya chanjo pia tulikua na maeneo maalumu 5 kama Shule ambayo tuliyatumia ili kuwasogelea Wananchi na kutoa chanjo kwa Watoto kusudiwa, tunashukuru muitikio kwa Wananchi ulikua mkubwa sana" amesema Nchimbi

Aidha Bw. Nchimbi richa ya kufanikiwa katika zoezi zima la utoaji chanjo, Sekta ya Afya ilifanikiwa kujua kuna kundi la Watoto 136 halikuwahi kupata chanjo ya aina yoyote katika kipindi chote cha maisha mpaka walipofikiwa, hivyo walipewa chanjo ya Surua na utaratibu wa kuwapa chanjo zingine ambazo hawakuwahi kupata zilifanyika ili kusaidia kuimarisha kinga zao za mwili


Kwa niaba ya Divisheni ya Afya Bw. Thomas Nchimbi ametoa pongezi na Shukrani kwa Wizara ya Afya kwa kutoa chanjo ambapo Wilaya ya Ngorongoro pekee ilipokea dozi 54, 020 za chanjo


 "tunaishukuru Wizara ya Afya inayoongozwa na Mhe. Ummy Mwalimu kutupatia dozi za chanjo pamoja na fedha za kutosha kwaajili ya kutekeleza na kukamilisha zoezi zima la utoaji chanjo ndani ya Wilaya ya Ngorongoro"-Nchimbi


Bw. Nchimbi amendelea kutoa shukrani kwa uongozi mzima wa Wilaya ya Ngorongoro kuanzia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri Wilaya ya Ngorongoro kwa ushirikiano wa karibu walioutoa wakati wote wa utekelezaji wa zoezi zima la utoaji chanjo kuanzia siku ya kwanza mpaka ya siku nne

Pamoja na hayo Nchimbi amesema kuwa Divisheni ya Afya Wilaya ya Ngorongoro inatambua mchango wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kwa kutoa magari matatu, pamoja na lita 1000 za mafuta katika kukamilisha zoezi la utoaji chanjo kwa Watoto wanaoishi tarafa ya Ngorongoro


Kulingana na takwimu Wilaya ya Ngorongoro imeshika nafasi ya kwanza katika zoezi zima la utoaji chanjo ya surua ndani ya Mkoa wa Arusha na nafasi ya nane kitaifa ambapo zoezi la utoaji chanjo Wilaya ya Ngorongoro limetekelezwa kwa asilimia 136


Aidha Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro imetoa shukrani na kuwapongeza Wananchi kwa ushiriano waliyoutoa wakati wote wa utekelezaji wa zoezi hili, pia imeipongeza Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Dkt. Revocatus Ndyekobora kupitia Divisheni ya Afya na Wahudumu wote wa Afya kwa kufanikisha zoezi zima la utoaji chanjo kwa mafanikio

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • WILAYA YA NGORONGORO YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI WA ΜΑΡΑΤΟ ΝA KUPATA HATI SAFI.

    June 11, 2025
  • NGORONGORO YANG'ARA MASHINDANO YA RIADHA UMITASHUMTA MKOA 2025.

    June 03, 2025
  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI CHANJO NA DAWA KINGA ZA MAGOJWA YA MINYOO NA TRAKOMA HALMASHAURI YA WILAYA YA NGORONGORO.

    May 30, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI WILAYANI NGORONGORO

    May 16, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.