• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhamira
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji na Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba za Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Kata
      • Loliondo
        • Ololosokwan
        • Soitsambu
        • Enguserosambu
        • Maalon
        • Oloirien Magaiduru
        • Piyaya
        • Orgosorok
        • Oloipir
        • Arash
      • Ngorongoro
        • Alailelai
        • Naiyobi
        • Olbalbal
        • Nainokanoka
        • Kakesio
        • Ngorongoro
        • Eyasi
        • Endulen
        • Ngoile
        • Alaitolei
        • Misigyo
      • Sale
        • Sale
        • Malambo
        • Digodigo
        • Oldonyosambu
        • Samunge
        • Pinyinyi
        • Kirangi
        • Engaresero
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezw
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

Ziara ya Mheshimiwa Januari Makamba (Mb) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira katika Wilaya Ngorongoro

Posted on: March 30th, 2017

Ziara ya Mheshimiwa Januari Makamba (Mb) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira katika Wilaya Ngorongoro.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira Mheshimiwa January Makamba (Mb) alifanya ziara Wilayani tarehe 28 na 29 mwezi Machi 2017. Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Waziri aliweza kutembelea Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCA) katika Tarafa ya Ngorongoro na Ziwa Natron katika Tarafa ya Sale. Ziara hiyo ilikuwa na malengo yafuatayo:-

  • Kukagua shughuli za uhifadhi wa Mazingira zinazotekelezwa katika Wilaya.
  • Kufuatilia na kusisitiza utekelezaji wa sheria za mazingira ikiwa ni pamoja na kusaidia Wilaya katika utekelezaji wa Sheria hizo.
  • Kuona ni kwa jinsi gani Wizara itakavyoweza kujenga uwezo mkubwa Zaidi katika kusimamia na kutekeleza Sheria za Mazingira kwa lengo la kusimamia Hifadhi za Mazingira.

Akiwa katika Tarafa ya Ngorongoro, Mheshimiwa Waziri alitoa maagizo yafuatayo:-

  • Kuchukua hatua za haraka ili kudhibiti mimea inayohatarisha uoto wa asili katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
  • kuundwa kwa jopo la wataalamu kutoka Tume ya Sayansi na Tecknolojia, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira, Hifadhi za Taifa za Tanzania, Wizara ya Kilimo na Mifugo na Mamlaka ya Ngorongoro kufanya utafiti wa kina na wa kisayansi wa kubaini mbinu mpya za kupambana na mimea hiyo vamizi.
  • kufanyika kwa ukaguzi wa kimkakati wa Mazingira utakaojumuisha Wilaya nzima ya Ngorongoro na kuitaka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kutekeleza wajibu huo mapema. Ukaguzi huo wa kimkakati wa kimazingira kwa Wilaya hiyo unatazamiwa kutoa mtazamo wa hali ya mazingira kwa miaka hamsini ijayo.
  • kufanyika kwa Tathmini ya Athari kwa Mazingira ama Ukaguzi wa Mazingira katika Hotel zote zilizopo eneo hilo na kulitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kuwaadhibu kwa kuwatoza faini wahusika wote ambao hawana vyeti hivyo.

Akiwa katika Tarafa ya Sale ambalo ni eneo la Ziwa Natron, maarufu kwa mazalia ya flamingo ‘Laser Flamingo’, uwepo wa madini aina ya magadi soda, uwepo wa chemchem ya maji moto na pia ni sehemu ya miongoni mwa Milima ya volcano hai ya Oldonyo Lengai.

Mheshimiwa Waziri aliweza kukagua shughuli za utunzaji na uhifadhi wa mazingira. Mheshimiwa Waziri alipokea taarifa fupi ya shughuli za utunzaji wa mazingira iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya Bwana Baltazary Victor Kaiza. Pamoja na mambo mengine taarifa hiyo iliainisha changamoto mbalimbali za mazingira katika Wilaya ikiwa ni pamoja na:

  • Hali ya ukame
  • Uvamizi wa Misitu na vyanzo vya maji.
  • Uchimbaji holela wa madini
  • Kukatwa kwa miti kwa ajili ya shughuli za kuchoma mikaa zisizo endelevu.

Baada ya kupokea taarifa, Mheshimiwa Waziri alipongeza jitihada kubwa zinazofanywa na Wilaya katika kuhakikisha kuwa shughuli za uhifadhi na utunzaji wa mazingira zinapewa kipaumbele kikubwa. Aidha Mheshimiwa Waziri aliweza kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Engaresero kupitia Mkutano wa hadhara. Mheshimiwa Waziri alisisitiza shughuli za utunzaji wa mazingira na maliasili kwa ujumla na kuona uwepo wa Mpango wa serikali kuandaa mradi wa kulinda na kuhifadhi Ziwa Natron. Mradi huo utahusisha maslahi mapana ya wananchi waishio pembezoni mwa ziwa hasa kwa kutumia rasilimali zipatikanazo katika ziwa hilo.  

Matangazo

  • TANGAZO LA RATIBA YA UCHAGUZI NA UANDIKISHAJI WA UCHAGUZI. September 26, 2024
  • TANGAZO LA UANDIKISHAJI VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA. October 01, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI.2. September 29, 2024
  • MATOKEO YA USILI WATENDAJI WA KIJIJI. September 29, 2024
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • NGORONGORO MSTARI WA MBELE KUHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

    May 09, 2025
  • KISIMA CHA MAJI SAFI KUCHIMBWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA NGORONGORO

    April 25, 2025
  • ZIARA YA MWENYEKITI WA HALMASHAURI TARAFA YA NGORONGORO.

    April 28, 2025
  • WANAFUNZI 576 WA KIDATO CHA SITA KUFANYA MTIHANI WA TAIFA NGORONGORO.

    May 06, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Afisa kilimo Ngorongoro aeleza na kufafanua namna ya kupata mazao yenye afya na mbegu bora kutumia katika kilimo.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Upimaji darasa la Nne 2019
  • Taarifa na Matangazo
  • Mikataba na Miongozo
  • machapisho mbalimbali
  • Habari kwa umma
  • Taarifa kwa Umma
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI JUNE 2019.
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 NGORONGORO

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Rais
  • Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
  • NGORONGORO DC YOUTUBE CHANEL
  • MATOKEO YA UPIMAJI DARASA LA NNE 2019 WILAYA YA NGORONGORO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 NDC . Haki zote zimehifadhiwa.